Idara ya Ufamasia
(Pharmaceutical Sciences)
Karibu katika Idara ya Ufamasia. Tunatoa elimu bora ya sayansi ya dawa, utayarishaji, na usimamizi wa dawa kwa viwango vya kimataifa.
Kozi ya Ufamasia (Pharmaceutical Sciences)
Ufamasia (Pharmacy) ni fani inayohusika na sayansi ya dawa, kuanzia ugunduzi, uzalishaji, udhibiti wa ubora, hadi matumizi salama ya dawa kwa wagonjwa. Katika Kolandoto College, tunatoa mafunzo yanayomjengea mwanafunzi ujuzi wa kitaalamu katika kusimamia dawa na kutoa huduma bora za afya.
Majukumu ya Mfamasia
- Kutoa Dawa (Dispensing): Kutoa dawa kwa usahihi kulingana na maelekezo ya daktari.
- Ushauri wa Dawa: Kuelimisha wagonjwa kuhusu matumizi sahihi na athari za dawa.
- Usimamizi wa Dawa: Kuhakikisha dawa zinahifadhiwa vizuri na hazijaisha muda wake.
Fursa za Ajira
- Maduka ya Dawa (Community Pharmacies) na Hospitali.
- Viwanda vya Dawa na Uzalishaji.
- Taasisi za Udhibiti (kama TMDA) na Utafiti.
Fursa za Kujiendeleza (Career Advancement)
- Bachelor of Pharmacy (BPharm): Shahada ya Ufamasia ili kuwa Mfamasia Kamili (Pharmacist).
- Industrial Pharmacy: Kubobea katika uzalishaji wa dawa viwandani.
- Clinical Pharmacy: Kubobea katika matumizi ya dawa wodini kwa wagonjwa.
Sifa na Mahitaji Maalum
Sifa za Kitaaluma
Kidato cha Nne (CSEE) chenye ufaulu wa "D" nne (4). Lazima zihusishe masomo yasiyo ya dini: Chemistry na Biology (Ni Muhimu), pamoja na Physics/Engineering Sciences.
* Ufaulu katika English na Mathematics ni nyongeza nzuri.
Mahitaji ya Mwanafunzi
- Laptop au Smartphone (Kwa ajili ya kujifunzia)
- Scientific Calculator
- Koti la Maabara (White Lab Coat)
- Ream Paper 2 (Double A) & 1 Box of Surgical Gloves
- Daftari na Vifaa vya Kuandikia
Malazi (Accommodation)
Ada ya Hostel ni TZS 300,000 kwa mwaka. Mwanafunzi aje na:
- Godoro (Size 2.5" × 6")
- Ndoo (Bucket)
- Chandarua (Mosquito Net)
- Vyombo vya chakula (Hotpot)
Tayari kukidhi vigezo?
Wasilisha maombi yako sasa hivi mkondoni bila ada yoyote ya awali.
Jaza Fomu OnlineAda na Michango (Mwaka 2026)
✓ Confirmed 2026 IntakeAda ya Mafunzo (Tuition Fee)
Jumla kwa mwaka mmojaJinsi ya Kulipa (Payment Instructions)
1. Kwa Tuition Fee & Michango (Accommodation/Exams):
2. Kwa Direct Costs (Uniform, NHIF, n.k.):
Lazima upate Control Number kabla ya kulipa. Piga simu Ofisi ya Uhasibu:
0621 521 2784 | 0615 801 748Fomu ya Kujiunga (Joining Instruction)
Bonyeza "Angalia Hapa" ili kuona PDF moja kwa moja.
Pakua Fomu ya Kujiunga
Fomu hii ina maelekezo yote ya kujiunga (Joining Instructions), fomu ya matibabu (Medical Form), na utaratibu wa malipo.
Vitu vilivyomo kwenye Fomu
- Joining Instructions (Maelekezo ya Kujiunga)
- Medical Form (Fomu ya Matibabu)
- Utaratibu wa Malipo na Akaunti
- Orodha ya Vifaa vya Kuleta
- Tarehe ya Kuripoti
Ukubwa wa Faili: ~2MB | Format: PDF
Mawasiliano ya Idara
Mawasiliano Muhimu
Mkuu wa Idara
0757 164 416Mahali Tulipo
Kolandoto College ipo kilomita 18 kutoka Mwanza Jiji, karibu na Mahakama ya Mwanzo Kisesa.
info@kchsm.ac.tz